Bukobawadau

KITUO CHA MAFUTA CHA MWENDO WA SAA CHANUSURIKA KUUNGUA MOTO USIKU HUU

Kituo cha mafuta cha mwendo wa saa kinacho milikiwa na Mdau Rajesh (Raju) Pater pichani kimenusurika kuungua kwa moto kutokana na moto kuzuka pembezoni mwa kituo hicho wakati gari la likiwa linapakua mafuta na kushika moto
 Juhudi za kuzima moto  kwa kutumia ndoo za mchanga na maji  kutoka kwa majirani zimesaidia kabla ya zima moto kufika kwenye eneo la tukio.
 Moto ulishika kwenye tank la gari la mafuta lililokua likipakua ndipo dreva akawahi kuliondoa .
Sehemu wa mashuhuda wa janga hili  wakiwa hawana la kusema.
Paipu za mafuta baada ya kuzimwa.
 Gari la zima moto likiwa limefika eneo la tukio.
Wafanyakazi wa zima moto wakijaribu kutafuta chanzo kwa kuchimba njia za  matank ya kuhifadhi mafuta.
 Napata ugumu kuelezea kilichotokea , ikiwa paipu za mafuta zimeungua na bado ni salama nisije kukuchanganyia story ila ukweli ndio huu hapa!!!
Kituo hiki kipo umbali wa km 5 nje kidigo ya mji wa Bukoba barabara ya Mtukula
Hivi ndivyo moto ulivyoshika na kuunguza nyasi zilizo zunguka eneo la kituo cha mwendo wa saa
 Maeneo yaliopatwa na moto...!!!
Ndg Mniru ni mmoja wa wafanyakazi wa kituo hiki akijaribu kutoa ufafanuzi kwa Mdau Katete Kinobi juu ya kile kilichotokea.
Meneja wa kituo hiki Mdau  Sunny Shabalala akijadili jambo na mmiliki wa gari  Mdau Mzee Sadru kulia.
Kila mtu haamini anacho ambiwa ni kama ajabu mafuta ya petrol kuzimika!!!!
 Pongezi kwa dereva  Mdau Shaffi Sadru (kushoto) kwa ujasiri, uzalendo na umahiri wa kuondoa gari wakati tenk  limeanza kushika moto!!!

NI BUKOBAWADAU PEKEE KWA HABARI ZA PAPO KWA PAPO!!!
Next Post Previous Post
Bukobawadau