Bukobawadau

Mahakama ya Wilaya ya Bukoba leo tarehe 11


Mahakama ya Wilaya ya Bukoba leo tarehe 11/09/2013 imemhukumu Kifungo cha Miaka 30 mtu mmoja anayeitwa BAGAICHWAKI S/0 MATHAYO Umri miaka 40 kwa kosa la kubaka kinyume na kifungu cha 130(2)(e) na 131(1) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu [Sura 16 Marejeo 2002]. Katika kesi ya jinai Na. na 33/2013.
Maelezo ya Shtaka: Mshtakiwa mnamo Tarehe 18 Mwezi Aprili Mwaka 2013 maeneo ya Nyamkazi katika Manispaa ya Bukoba Mkoa wa Kagera, alifanya mapenzi na msichana xxxx ambaye ni msichana mwenye umri wa miaka 15.
Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Bukoba Charles Uiso aliridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani na mashahidi wa upande wa mashtaka wakiongozwa na Wakili wa Serikali Chema Maswi Mbena, ikiwa ni pamoja na mhanga mwenyewe ambaye alieleza jinsi alivyofanya mapenzi na mshtakiwa katika chumba cha mshtakiwa tarehe 18/04/2013, ambapo wakiendelea kufanya kitendo hicho ndipo walipotokea majirani pamoja na mzazi wa msichana huyo ambao walimuona akiingia nyumbani kwa mshtakiwa. Mahakama pia ilipokea kielelezo cha hati ya matibabu (PF.3) kilichotolewa na mhanga (victim).
Utetezi:Mahakama haikuridhika na utetezi wa mshtakiwa kuwa alibambikiziwa kesi hiyo kwakuwa alikuwa anamdai sh. 50,000/= baba wa Mhanga ambapo Mahakama ilisema kuwa utetezi huo ni wa kutunga “afterthought” kwani alipopewa nafasi ya kumuuliza maswali baba wa mhanga hakuuliza kuhusu kiasi hicho cha pesa anachomdai.
Uamuzi:Mahakama iliridhika kuwa upande wa mashtaka umethibitisha shtaka bila kuacha shaka lolote na hivyo ikamtia hatiani mshtakiwa.
Kumbukumbu za nyuma za uhalifu za Mshtakiwa:Upande wa mashtaka haukuwa na kumbukumbu zozote za uhalifu za mshtakiwa hata hivyo uliiomba mahakama kutoa adhabu kali kwa mshtakiwa kwani tabia ya watu wazima wenye umri mkubwa kama mshtakiwa imekuwa sugu katika jamii na hivyo adhabu kali haina budi kutolewa ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia hizo.
Sababu za Shufaa (Mitigation): Mshtakiwa hakusema lolote juu ya kuiomba mahakama impunguzie adhabu

Kifungo: Miaka 30
Next Post Previous Post
Bukobawadau