Bukobawadau

ULINZI WA MAKACHERO WA POLISI WAMPA ZITTO UJASIRI WA KUTAJA MAJINA YA WALIOFICHA PESA USWIZI

Baada ya kutembea na list mfukoni kwa miaka, Mh. Zitto amefunguka, amesema yupo tayari hata kuuawa kama sababu yenyewe ni kuokoa fedha za watanzania. Amekiri kuwa walioficha fedha nje wamezoroyesha uchumi wa nchi. Zitto atawataja Mafisadi na wezi walioficha fedha nje kwenye kikao kijacho cha bunge.

Tunampongeza kwa ujasiri huo, atleast anaweza kurudisha imani kwa wananchi.

Zitto amesema hatuwezi kukomboa nchi hii bila chadema, mambo yanayotokea kamati kuu itafanya jitihada kuyamaliza ili tuwatetee watanzania.

Kumtaja Mwizi hadharani haihitaji itifaki.
Hatua hii imekuja baada ya Zitto Kabwe kupewa ulinzi wa kikachero utakaohakikisha hadhuriki na mahasimu wake wa kisiasa na wanaolenga kukwamisha vita dhidi ya uhujumu wa kodi za wananchi na uchumi wa nchi.

Source: DW
Next Post Previous Post
Bukobawadau