Bukobawadau

NALPHIN HOTEL & NIGHT CLUB YAZINDULIWA RASMI NA MH.BALOZI KHAMIS KAGASHEKI,DEC 5.

 Mkurugenzi wa Ukumbi mpya wakisasa kabisa wa 'Nalphin Hotel &Night Club .Mr Nafu  na mkewe pichani katikati wakiwasha mishumaa juu ya Keki ikiwa ni hatua ya Uzinduzi wa Ukumbi  wa Ukumbi huo uliopo Wilayani Muleba.
 Mgeni rasmi ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Mh. Balozi Khamis Kagasheki aka 'swahiba'  (pichani Kushoto) akishiriki tukio la kukata Keki  kuashiria kuwa sasa Ukumbi wa 'Nalphin Hotel & Night Club  ,ukumbi wenye kila sifa umezinduliwa rasmi ,Ni tukio lililo fanika Usiku wa Jana Ijumaa Dec 5,2014 na kuhudhuriwa na mamia ya watu.
Kushoto ni mmoja wa  washereshaji wa Shughuli hii,msanii maarufu wa filamu za Kibongo, Elizabeth Michael 'Lulu' akionyesha umahiri katika tasnia ya kipaza,kushika 'maiki'
Pichani anaonekana Mmoja wa washika dau wa karibu sana na Mr.Nafu akifanya Ukodak kupata matukio.
Vyombo mbalimbali vya habari vimeweza kushiriki kikamilifu Uzinduzi wa mradi huo
Taswira Ukumbini.
Shughuli ilitanguliwa na Sala iliyo ongozwa na mchungaji pichani
Mh. Balozi Khamis Kagasheki ,Mgeni rasmi katika Uzinduzi wa Ukumbi na Hotel Mpya na ya Kisasa akitoa maneno ya shukrani na pongezi kwa Mkurugenzi Mr Nafu na familia yake  kwa kuamua kuwekeza, Uzinduzi huu umefanyika Usiku wa kuamkia leo  katika Ukumbi huo wa Nalphin hotel & Night Club  uliopo Wilayani Muleba.
 Mgeni rasmi Mbunge wa Jimbo la Bukoba Mjini Balozi Khamis Kagasheki akiendelea kuongea.
Taswira mbalimbali Ukumbini.
 Sehemu ya Wageni waalikwa Ukumbini
Wadau mbele ya Camera yetu ukumbini
Mrs Gama na Mrs Makoko ni sehemu ya waalikwa katika uzinduzi huu
 Mwinjuma Muumini akionesha umahiri wake
 Wanenguaji wa Bendi ya Muumin Mwinjuma 'Kocha wa Dunia'
 Jukwaa likishambuliwa na Wanamuziki wakiongozwa na Mkongwe wa muziki wa dansi, Mwinjuma Muumini almaarufu kama Kocha wa Dunia.
 Shabiki mzuka unapo panda
 Safu ya waimbaji wa Bendi ya Mwinjuma Muumini almaarufu kama Kocha wa Dunia.
Burudani kutoka kwa wasanii wa Jijini Mwanza.
 'Mashigonge Group' wakali wa burudani ya asili kanda ya ziwa wakifanya yao
Katika kushow love na Bukobawadau
Sasa ni wakati wa kufungua champagne zisizo na Idadi ukumbini.
Miripuko ya hapa na pale yaani 'Ebyensinka'
 Anaonekana shwari bila stress wala nini anaonekana Mdau Jamal Kalumuna
 Kutoka Kemondo Bay pichani ni Mzee Hamdan(Baba Mnawar)
Hakika watu ni wengi kweli kweli.
Neno kutoka kwa Mr . Nafu Mkurugenzi wa Nalphin Hotel & Night Club
 Anaitwa Ruhi kutoka 'Rock City' ni mmoja wa ma emcee walioweza kusababisha tukio hili la kihistoria ndani ya Wilaya Muleba na Mkoa wa Kagera kiujumla.
Waalikwa ukumbini wakiendelea kupata kile kinacho stahili.
 Katika hali ya furaha anaonekana Eng. Jeremy pichani.
Mr. Rahm Kabemela na Mdaun Jamal (Jamco) Kalumuna
Mr.Khakiim Kichwabuta akisalimiana na Mkurugenzi Mr. Nafu
Mdau Khakiim Kichwabuta ambaye ni mshauri mkuu na mikakati endelevu juu ya shughuli nzima ya Uzinduzi wa Nalphin hotel &Night Club , pichani anasalimiana na Mgeni rasmi Mh. Balozi Khamis Kagasheki Mbunge wa Jimbo la bukoba mjini.
 Ni mwendo wa Vinywaji vya kila aina kwa Wageni wengi waalikwa walianza kuingia ukumbini majira ya Saa moja jioni.
 Home boy Amani Kabuga alisimama kama Mc mshereheshaji kwa kusaidiana na Msanii 'Dude'
Muonekano sehemu ya waalikwa mbalimbali.
 Sehemu ya waalikwa ,anaonekana Haji Adam Sued pichani wa pili kutoka kulia
 Wageni wanaendelea kuingia ukumbini
 Waalikwa Ukumbini.
Watu wakiendelea kufurahia uzinduzi wa Mradi  huu mkubwa kabisa Wilayani Muleba
 Pichani kushoto ni Meneja uendeshaji wa kampuni ya utalii ya Kiroyera,Ndugu William Rutta
 Mr. Jumanne kama anavyo onekana pichani akiwa kajipanga na Cassio mikononi ajili ya matukio
Muonekano wa wadau katika hali ya kiwango.
Kulia ni  muigizaji maarufu wa filamu Bongo, Kulwa Kikumba maarufu kama 'Dude' au Yahaya.
Kushoto ni Mr Sued Juma Kagasheki akifuatiwa na Mzee Abdul Sued (Kananga)
 Mpambanaji mtu wa (events)Jamal Jamco Kalumuna.
 Pongezi zikimiminika kwa Mkurugenzi wa Nalphin hotel & Night Club
Wanakamati  muda mchache kabla ya Utambulisho
Anaitwa Samson Alfred Makoti aka 'Tolo' akiendelea kuwajibika
Mr Didas Zimbihile akiteta jambo na Mh. Balozi Khamis Kagasheki
 Mikono ya pongezi ikiendelea...

Mzee akitoa shukrani zake kwa Mgeni rasmi kwa namna ya pekee na kwa dhati kabisa
 Taswira meza mbalimbali ikiwa ni Shughuli ya Uzinduzi wa 'Nalphin Hotel & Night Club.
 Futuhi wakiwajibika.
 Mc Elizabeth Michael maarufu kama Lulu full kicheko
 Ndani ya Mji mdogo wa Muleba pichani ni sehemu ya Wadau walioweza kuhudhuria Uzinduzi huu.
 Mdau akicheck na Camera wetu ukumbini.
MUHIMU :BUKOBAWADAU BOG tunafurahia kuwa na uwezo wa kukupa nafasi ya matangazo katika mtandao wetu pia kwa taarifa au shughuli yotote ili kufikia idadi ya watu unaotaka kokote dunia waweza kuwasiliana nasi kupitia namba +255 784 505045,0754 505043,0715 505043 ,0768 397241
 Upande wa Night Club watu 'full Kadansee'
 Muonekano wa Kaunta ya Chini ndani ya Nalphit Night Club
 Ya mambo ya Club kwa mkutasali... Endelea kuwa nasi kwa Storo kamili na picha zaidi
 DJ  kwa mtambo akiwarusha watu waliokuja kujipa raha kwa mara ya kwanza kabisa hapa Nalphin
Tutaendelea zaidi kwa mtiririko Mzuri wa Matukio, Japo unaweza kuona matukio zaidi ya picha zipatazo 200 kuopitia Ukurasa wetu wa facebook ingia hapa>>Bukobawadau Entertainment Media
Next Post Previous Post
Bukobawadau