Bukobawadau

BALOZI WA CHINA NCHINI TANZANIA AFANYA ZIARA MKOANI KAGERA KUKAGUA ENEO LA KUJENGA CHUO CHA KISASA CHA UFUNDI (VETA) NA KUONA FURSA ZA UWEKEZAJI KATIKA MKOA

Balozi wa China nchini Tanzania LU Youqing amewasili mkoani Kagera  leo  alasili tarehe 27/01/2015 kwa ziara ya siku mbili kukagua eneo  lililotengwa na serikali ya mkoa kwa ajili ya kujenga chuo cha Ufundi (VETA) cha Kitaifa kilichohaidiwa na serikali ya China wakati wa ziara ya Rais Kikwete nchini humo mwaka jana Oktoba 2014.

Akimkaribisha mkoani Kagera Mkuu wa Mkoa John Mongella alimweleza Balozi LU kuwa mkoa wa Kagera una fursa nyingi za uwekezaji ambazo ni pamoja na uwekezaji katika viwanda vidogo vidogo vya kusindika bidhaa mbalimbali ili kuinua uchumi wananchi na mkoa kwa ujumla.

Bw. Mongella alimwomba Balozi LU kufikiria kuleta wataalamu wa afya hasa madaktari kutoka nchini mwake hususani katika haospitali ya Rufaa ya mkoa ili kutoa huduma kwani mkoa upo mbali sana na hospitali za Rufaa za taifa jambo ambalo huleta usumbufu kwa wagojwa wanaohitaji huduma za hospitali za rufaa.

Balozi LU katika kutoa salaamu zake alisema kuwa  amefurahi kufika mkoani Kagera kwa mara ya pili na akasifu mkoa kwa kuwa na hali nzuri ya hewa na kubarikiwa katika nyanja mbalimbali za kiuchumi. Aidha, alisema kutokana na urafiki wa nchi mbili za Tanzania na China amefurahi kuwa sasa kutakuwa na alama ya urafiki huo katika mkoa wa Kagera.

Pamoja na kuusifia Mkoa wa Kagera imeisifia serikali ya Tanzania kwa kutekeleza miradi ya maendeleo akisema kuwa  ukipita mikoani unaona mabadiliko makubwa kuliko ilivyokuwa hapo nyuma.  Ambapo alisema kuwa serikali ya China imewekeza na kutekeleza miradi ya maendeleo nchini Tanzania yenye thamani ya bilioni 3.15  dolla za kimarekani  kwa mwaka  2013/2014.

Balozi LU alitembelea kiwanja cha hekta 26,000 kilichopo eneo la Kahororo katika Halamashauri ya Manispaa ya Bukoba ambapo chuo cha ufundi (VETA) kitajengwa na kujionea mwenyewa kitakapojengwa chuo hicho. Pia alitembelea shule ya Mgeza Mseto ambako aliwahi kutembelea na kutoa msaada wa komputa ili kuona wanafunzi wa shule hiyo maendeleo yao.

Katika shule ya msingi Mgeza Mseto yenye wanafunzi wa bweni na kutwa pia inapokea watoto wa aina tatu, watoto wenye albinisimu, watoto wenye ulemavu wa viungo, na watoto wa kawaida,  Balozi LU alisema amefurahi kuwaona tena na kuhaidi kutoa msaada zaidi wa komputa ili watoto waweze kila mmoja kujifunza komputa.

Katika maelezo yake Balozi LU aliufananisha mkoa wa Kagera na Jimbo la Chandog la nchini China na kusema kuwa atahakikisha unaungaisha urafiki kati ya mkoa wa Kagera na jimbo hilo ili kuleta maendeleo zaidi Kagera. Vilevile alisema atahakikisha anfanya mpango wa Tanzania hasa mkoa wa Kagera unakuwa na utaratibu wa kubadilishana walimu kutoka nchini China.

Maeneo ya uwekezaji ambayo mkoa umeyatenga kwa ajili ya uwekezaji ni pamoja na Kilimo cha kisasa katika maeneo mbalimbali, Ufugaji wa kisasa wa samaki, Ujenzi wa bandari ya Kemondo(contena terminal)  na ufugaji wa kisasa wa nyuki pamoja na ujenzi wa chuo cha ufundi (VETA)
 Balozi LU akicheza nngoma uwanja wa ndege mara baada ya kuwasili
 Balozi LU akisaini kitabu cha wageni Bukoba airport
 Balozi LU akionyeshwa eneo litakapojengwa chuo
 Balozi LU akipokea zawadi toka kwa wanafunzi wa shule ya Mgeza Mseto
 Balozi LU akipokea zawadi toka kwa wanafunzi wa shule ya Mgeza Mseto
 Katika picha ya pamoja.
Next Post Previous Post
Bukobawadau