Bukobawadau

MIEMBENI BUKOBA WAANZA KWA MWAMKO KUJIANDIKISHA KATIKA DAFTRARI LA WAPIGA KURA KWA MFUMO WA KIELEKTRONIKI

Mr. Rahym Kabyemela akishiriki zoezi la kujiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura lililo anza rasmi kwa mwamko mkubwa na limekwenda vizuri , siku ya leo Jumanne May 21,2015 katika kata ya Miembeni Manispaa ya Bukoba.
Blogger Mc Baraka akiweka sahihi yake mara baada ya kujiandikisha katika daftari hilo ili kuweza kushiriki vyema katika zoezi la kupiga kura katika uchaguzi mkuu.
 Hawa ni Watu walioanza kupanga mstari majira ya saa moja asubuhi kufikia sasa majira ya saa 12 jioni wakati picha hii inachukuliwa.
 Mdau Badru Kagasheki akishiriki zoezi la uboreshaji wa daftari la kudumu la wapiga kura kupitia mfumo wa BVR.
 Watu wakiwa kwenye mstari kwa ajili ya kushiriki zoezi hilo
 Sehemu ya wananchi wakiwa kwenye mstari kwa ajili ya kujiandikisha katika Daftari la kupiga kura.
 Wadau pichani wakiwa tayari kushiriki kikamilifu katika uandikishaji wa daftari la kudumu la wapiga kura
 Zoezi la uandikishaji likiendelea.
 Dj Y na Dj Sley pichani wakisubiri utaratibu.
 Bi Subira ,Mama Hakhram pichani.
 Sehemu ya wakazi wa kati ya Miembeni wakiwa tayari kushiriki zoezi hilo
 Zoezi la uandikishaji katika Daftari la kudumu linaloendelea kwa wiki moja katika Ofisi za 'Labour 'zilizopo mtaa wa Jamhuri Miembeni.
Watendaji wa tume wakiendelea na zoezi la  wakiandikisha wapiga kura
 Mpaka mwisho wa tarehe ya leo May 21 zoezi hili la kuandikisha limeonekana kwenda vizuri
 Taswira nje ya Viwanja vya Ofisi za Idara ya Kazi zilizopo Miembeni Mjini Bukoba
Next Post Previous Post
Bukobawadau