Bukobawadau

VURUGU ZA KISIASA KARAGWE

Taarifa zinasema kuwa hali si hali katika kijiji cha Nyamiyaga Kata ya Bugomora wilayani Kyerwa vurugu kubwa zinaendelea kati ya watu wanaosadikiwa ni wafuasi wa vyama vya CCM NA CHADEMA.
Hali hiyo ya taflani imezukua mida ya saa 12 jioni ambapo mpaka sasa magari 3 yamevunjwa vioo na nyumba kadhaa kubomolewa.
Shuhuda wetu anatujuza kuwa tayari amewasiliana na Jeshi la polisi wa kituo kilichopo Mpakani mwa Tanzania na Uganda
Taarifa ya awali inasema vurugu hizo ni kufuatia misafara videdea vya wagombea kukutana eneo la nyamihanga sokoni Ikiwa mgombea wa CCM Ndugu Zzawadi Niclous Kazahura alikuwa na mkutano kijiji cha Nyamiaga alipo maliza mkutano aliondoka na kuwaacha wafuasi wake wakiendelea kuruka ngoma na muziki "mbele kwa mbele" hapo hapo eneo husika
Nae mgombea udiwani kupitia Chadema Bw Tulakile Twijuke Libent Aliyekuwa na mkutano katika kijiji cha Magoma ,mwisho wa mkutano wakitumia barabara moja yenye makutano na eneo la tukio yalipo makazi halisi ya mgombea huyo hapo ndipo hali ya sintofahamu ilipo jitokeza .
Endelea kuwa nasi kwa taarifa zaidi .
Next Post Previous Post
Bukobawadau