Bukobawadau

RWEGASIRA FC WASHINDA 1-0 DHIDI YA KIBETA

 Wenyeji wa michuana ya Rwegasira Cup timu yaRwegasira Fc ya Kitendaguro wametoka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Kibeta mchezo uliopigwa kwenye Uwanja wa chuo cha Afya Cha Kagemu.
Taswira kutoka Viwanja vya Chuo cha Afya Kagemu kilichopo Kata Kitendaguro Manispaa Bukoba
Ndugu  Edward Emmanuel Rwegasira  pichani kushoto mdhamini na mwandaaji wa michuano hiyo akifuatilia Mechi ya kumtafuta mshindi wa tatu kati ya timu yake wenyeji Rwegasira Fc na Kebeta Fc
Wapenzi wa Soka wakifuatilia mchezo wa Mashindano ya Rwegasira Cup yaliyoandaliwa na Mmoja wa Watoto wa Marehemu mzee Emmanuel Rwegasira aliyewahi kuwa Mbunge wa Bukoba Vijijini na Mwenyekiti wa CCM Wilaya Bukoba ni katika Uwanja wa Chuo cha Afya Kagemu Manispaa Bukoba.
 Viongozi wa timu Rwegasira Fc walioibuka kidedea kwa kuichapa bao 1-0  timu ya Kibeta Fc.
Mtanange ukiendelea Uwanjani
 Benchi la Wachezaji wa Timu ya Rwegasira Fc.

 Wachezaji wa timu ya Rwegasira Cup wakishangilia bao lao la Ushindi
Mchezo wa  fainali hizi unatalajiwa kufanyika Jioni ya leo Ijumaa kwa kuzikutanisha timu ya Bukoba Municipal Council (BMC) na Buhembe Fc
 Mchezaji wa Kibeta Fc akitibiwa ili arudi uwanjani
Wadau wa kamati ya maandalizi ya Michuano ya Rwegasira Cup
 Muendelezo wa matukio ya picha Uwanjani Rwegasira Fc 1-0 Kibeta Fc.
Mpambano wa kutafuta mshindi wa tatu,Michuano ya Rwegasira CUP 
 Wakati Mgeni Rasmi ambaye ni mdhamini wa Michuano hii Ndugu  Edward Emmanuel Rwegasira akisalimiana na Wachezaji na Viongozi wa timu ya Rwegasira Fc.
 Katika picha ya Pamoja na Wachezaji wa Kibeta Fc.
Mchezo wa  fainali za  Rwegasira Cup unatalajiwa kufanyika  leo Ijumaa July 12,2019 saa 10:00 Jioni kwa kuzikutanisha timu ya Bukoba Municipal Council (BMC) na Buhembe Fc


Next Post Previous Post
Bukobawadau