Bukobawadau

MKUTANO MKUU WA KKKT 2023 - UCHAGUZI MKUU

Duru ya kwanza ya kupiga kura imemalizika. Matokeo ni kama ifuatavyo;
Jumla ya kura zilizopigwa 253,
1. Askofu Malasusa kura 90,
2. Askofu Keshomshahara kura 83,
3. Askofu Fihavango kura 69
Kura zilizoharibika 11.
 Kwa kuwa hakuna aliyepata theluthi mbili ya kura kwa mujibu wa Katiba ya KKKT, washindi wawili wa juu watarudia kupigiwa kura. Kwahiyo zoezi la kura linarudiwa baina ya Askofu Malasusa na Askofu Keshomshahara.
Ikiwa kati ya hao wawili hakuna atakayefikisha theluthi mbili ya kura, basi kura zitapigwa tena kwa awamu ya tatu na atakayepata kura nyingi (simple majority) ndiye atatangazwa Mshindi. Hivyo basi Mkuu mpya wa KKKT kutangazwa muda mfupi ujao. Kama sio Askofu Dr.Keshomshahara basi ni Askofu Dr.Malasusa.!

 

Next Post Previous Post
Bukobawadau